٢٣

Na kwa yakini tulimtuma Musa pamoja na Ishara zetu na uthibitisho ulio wazi,
٢٤
Kumwendea Firauni na Hamana na Qaruni, wakasema: Huyu ni mchawi, mwongo mkubwa.
٢٥
Basi alipo waletea Haki inayo toka kwetu, walisema: Waueni watoto wanaume wa wale walio muamini na wawacheni hai wanawake wao. Na haviwi vitimbi vya makafiri ila katika upotovu.
Notes placeholders